Wednesday 10 June 2015

" Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio ; Bali sasa jicho langu linakuona ." Ayubu 42:5

Kama ambavyo mtumishi wa Mungu Ayubu alivyosema hivyo ndivyo wana EAGT CITY CENTRE TUNASEMA LEO!!!

Ama kwa hakika tumemuona Mungu akifanya na ataendelea kufanya maana tulikotoka ni mbali kuliko tunakokwenda...!!!

Kwa takribani miaka mitano sasa tumekuwa tukiabudu katika Viwanja vya Maonesho vya Mwl Julius Kambarage Nyerere ( Sabababa) huku tukiwa na shauku ya kutaka kumiliki eneo letu ambapo tutajenga nyumba ya kumuabudu Mungu wetu pasipo bughudha.

Hakika Mungu amejibu maombi yetu kwa kutupa eneo katika eneo la MTONI MTONGANII karibu kabisa na Daraja la  Reli ya Tazara .....

Eneo hili  jipya lina  uwezo wa kuchukua takriban waumini 2,500 , na kuna mpango  endelevu ambao utawezesha upanuzi wa eneo hili hata kuweza  kuchukua jumla ya waumini 7,200.  Na hapo ndipo EAGT City Centre itadumu

Kikosi cha Bendi ya Jeshi la Polisi Tanzania kikiongoza maandamano kuelekea katika kanisa jipya .. 


Umati mkubwa wa waumini wa kanisa la EAGT CITY CENTER ukiongozwa na Mchungaji Florian Katunzi.



MChungaji Katunzi akiongoza msafara kuelekea lilipo kanisa jipya eneo la MTONI MTONGANI  jirani na reli ya Tazara.




Mwandishi na mtangazaji wa Radio WAPO Angelina Lukindo akifanya kazi yake wakati wa masafara..








Viongozi wa kanisa wakiwa wametangulia mbele  ili kuhakikisha mambo yanakwenda kwa utaratibu.


Waumini wakiwa wamebeba viti ambavyo watatumia katika kanisa hili jipya.



Mbeba maono na Mchungaji wa kanisa hili akikata utepe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa kanisa hili.

Viongozi mbalimbali waliokuwepo katika zoezi hilo

Umati wa waumini wakiwa ndani ya kanisa.

Unaweza pia kuwa sehemu ya baraka hizi kwa kutoa mchango wako utakaofanikisha kufikia lengo la ujazo wa watu 7,200 ndani ya miaka mitatu, kwa kuwasiliana na kutuma mchango wako moja kwa moja na Mchungaji Florian Josephat Katunzi kupitia namba 0754367826 ,  0784367826  au  0718267171.

Total Pageviews

Eagt City Centre Blog 2013. Powered by Blogger.

About Me

My photo
Jicho langu latoka machozi lisokome,wala haliachi;Hata BWANA atakapoangalia. Nakutazama toka mbinguni Maombolezo 3:49-50

Followers

Featured Posts

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget