Thursday 28 May 2015

SILAHA NANE ZA KUFUNGUA MILANGO NA MALANGO YALIYOFUNGWA MBELE YAKO;

SILAHA YA PILI

(ii) UWE HODARI TU
Silaha hii ni ya muhimu sana katika maombi yetu ya kufungua milango na malango maana mwenye imani itendayo kazi sharti awe hodari katika BWANA hata kama kuna magumu mbele yako unayapitia. Njia ya kuyashinda hayo ni kuwa hodari tu maana uhodari ndio unao fungua Milango na Malango. Hatukupewa roho ya woga bali ya uweza na nguvu katika Kristo Yesu. “Uwe hodari tu na ushujaa mwingi uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiache kwenda mkono wa kuume au wa kushoto upate kubarikiwa sana kila uendako.” Yoshua 1:7

Tunajifunza kwa mtume Petro alizama kwa kukosa imani thabiti, alipoona hofu moyoni mwake, akapoteza mwelekeo wa kiimani, akazama. Hofu ikiwa ndani mwa mkristo utapoteza uwezo wa kumiliki na kutawala. Maana hatuwezi kumiliki pasipo imani thabiti katika Mungu. “…Petro akajibu akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?...” Mathayo 14:22-32

Milango na Malango vitafunguliwa pale tunapokuwa na moyo wa ushujaa na uhodari. Watu wa Imani  sharti watoke waombe kwa nguvu zenye kuangusha ngome. Ukiwa na hofu na mashaka uwezi kusimama mbele ya maadui zako ukawashinda. “Bwana Mungu ndiye atakayevuka mbele yako; atawaangamiza mataifa haya mbele yako nawe utamiliki.” Kumbukumbu 31:3

Mbele yetu yuko Kristo Yesu, naye anasema atatufungulia milango na malango, na hao adui zetu wataangamizwa. Walio inuka juu yako watatiwa mkononi mwako na utayamiliki Malango na Milango ya adui zako. “Iweni hodari na moyo wa ushujaa; msiogope wala msihofu kwa maana Bwana Mungu wako yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe hatakupungukia wala kukuacha.” Kumbukumbu 31:6

“Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu nimuogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu nimuhofu nani? Watenda mabaya waliponikaribia wanile nyama yangu; watesi wangu na adui zangu walijikwaa wakaanguka. Jeshi lijapojipanga kupigana nami, moyo wangu hautaogopa vita vijaponitokea; hata hapo nitatumaini.” Zaburi 27:1-3

Imani pasipo shaka ndiyo inayofungua malango na milango hivyo mwombaji sharti uwe na imani isiyo na shaka. “Yesu akajibu akawaambia, amini nawaambia; mkiwa na Imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu lakini hata mkiuambia mlima huu ng’oka ukatupwe baharini itatendeka. Na yoyote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.” Mathayo  21:21-22

Milango na Malango yaliyofungwa yatafunguliwa kwa kuwa na moyo mkuu wa Imani isiyokuwa na shaka ndani mwake. Nasi tukiomba pasipo shaka yoyote hakika tutashinda. “Ila aombe kwa Imani pasipo shaka yoyote moyoni maana mwenye shaka nikama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo na kupeperushwa huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani atapokea kitu kwa Bwana. Mtu wa nia mbili husitasita katika njia zake zote.” Yakobo 1:6-8

Mtu mwenye mashaka, Mwenye hofu, Mtu mwoga na Mtu wa wasiwasi, ASIDHANI ATAPOKEA KITU KUTOKA KWA BWANA. Malango ya wengi yamefungwa mpaka sasa kwa sababu sio Hodari. Lazima mtu wa Mungu uwe Hodari tunajifunza kwa mfano wa Daudi alimshinda Goliathi sio kwa ujuzi  wa vita bali kwa Uhodari katika Mungu aliye hai. Hata mfalme Sauli alipomwambia Daudi huwezi kupigana na Mfilisti huyu maana amekuwa mtu wa vita tangu utotoni mwake. Lakini Daudi kwa imani alisema naweza kumpiga mfilisti huyu. “Daudi akamwambia Sauli, asizimie moyo mtu ye yote kwa ajili ya huyu; mimi mtumishimwako nitakwenda kupigana na mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi uwezi kumwendea mfilisti huyu upigane naye maana wewe u kijana tu; na huyu ni mtu wa vita tangu ujana wake. 1Samweli 17:32-33

Angalia Gidion ilibidi Mungu amwambie apunguze katika jeshi lake watu wote wenye hofu na wasiwasi, toka jeshi la askari thelathini na mbili elfu (32,000) mpaka askari mia tatu (300) walio Hodari tu. ”Kisha Yerubaali yaani Gidion na watu wote waliokuwa pamoja nae wakaondoka na mapema wakapiga kambi yao karibu na kijito cha Harod na kambi ya midiani ilikua upande wao wa kaskazini karibu na milima wa more bondeni. Bwana akamwambia Gidion, watu hawa walio pamoja nawe ni wengi mno hata nikawatie kwa Wamidiani katika mikono yao wasije Israeli wakajivuna juu yangu wakisema mkono wangu mwenyewe ndio ulioniokoa. Basi sasa enda tangaza habari masikioni mwa watu hawa na kusema, mtu awaye yeyote anayeogopa na kutetemeka na arudi aondoke katika mlima wa Gidon Gileadi, ndipo watu ishirini na mbili elfu wakarudi katika watu hao wakabaki watu elfu kumi. Bwana akamwambia Gidion hata sasa watu hawa ni wengi mno, uwalete chini majini name nitawajaribu huko kwaajili yako kasha itakuwa ya kwamba yule nitakaye kuambia huyu atakwenda pamoja nawe, ndipo atakwenda pamoja nawe na mtu yule nitakayekuambia huyu hatakwenda pamoja nawe basi mtu huyo hatakwenda. Basi akawaleta watu chini majini, Bwana akamwambia Gidion kila mtu atakaye yalamba maji kwa ulimi wake kama vile alambavyo mbwa huyo utamuweka kando kadhalika kila mtu apigaye mago ti kunywa na hesabu ya hao waliokunywa kwa kulambalamba wakipeleka mkono kinywani ilikua watu mia tatu bali watu wengine wote walipiga magoti kunywa maji. Bwana akamwambia Gidion kwa watu hawa mia tatu walioyalamba maji nitawaokoa name nitawatia wamidiani katika mikono yao, lakini watu hawa wote wengine na waende zao kila mtu mahali pake.” Waamuzi 7:1-7

Malango yako yatafunguliwa kwa Imani thabiti sio kwa wingi wa maneno, Yesu akamwambia Petro, Mbona umeona shaka moyoni mwako? Kikwazo na kizuizi kikuu ni mashaka hivyo ondoa mashaka na uwe hodari katika BWANA. “Si kwa uwezo wala si kwa nguvu bali kwa roho yangu asema BWANA. Nani wewe ee mlima mkubwa mbele ya Zerubabeli utakua nchi tambarare naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya neeme ilikalie.” Zekaria 4:6-7



1 comment:

  1. Casino in New York - Mapyro
    Casino 김포 출장마사지 is 화성 출장샵 a non-smoking casino 시흥 출장안마 located in Yonkers, NY. The casino is a non-smoking hotel and not a full-service casino. In the 고양 출장안마 photo, you can 양산 출장안마 see

    ReplyDelete

Total Pageviews

Eagt City Centre Blog 2013. Powered by Blogger.

About Me

My photo
Jicho langu latoka machozi lisokome,wala haliachi;Hata BWANA atakapoangalia. Nakutazama toka mbinguni Maombolezo 3:49-50

Followers

Featured Posts

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget