Thursday 21 April 2016



 Mchungaji askofu Katunzi akifundisha neno la Mungu ndani ya kanisa

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Faraja Ntaboba kutoka nchini Congo akihudumu ndani ya kanisa la EAGT City Center.
 kutoka kushoto ni mke wa askofu Katunzi,mchungaji Rachael Katundi


 Watoto wa kanisa la EAGT City Center wakimtukuza Mungu kwa njia ya uimbaji ndani ya kanisa wakati wa kutoa sadaka



 Msichana ambaye ni mwanafunzi wa shule Ya sekondani alifikishwa kanisani hapo wakati hawezi kutembea na baada ya maombi ameanza kufunguliwa na kuwekwa huru mbali na mateso na vifungo vya adui shetani.









Dada mwenye Nguo nyekundu katikati aliletwa na mama yake kanisani hapo na amefunguliwa na kuwekwa huru kwa jina la Yesu mtenda miujiza.



 Askofu Katunzi akitoa maelekezo wakati wa ibada maara baada ya kumaliza kufunduisha  neno la Mungu ndani ya kanisa hilo.




 Wauminiwakifuatilia maelezo ya mchungaji na Askofu Katunzi wakati wa ibada kujiombea mwenyewe kwa kuweka mikono juu ya kichwa.

 Viongozi na watendaji wa kanisa la EAGT City Center wakishikilia divai na mkate tayari kwa kushiriki.
 Askofu aKatunzi akisoma neno na kufanya maombi tayari kwa kushiriki meza ya Bwana ambapo wengi walifunguliwa na kuwekwa huru.
 waumini wa kanisa la EAGT wakiinua mikono juu kumshukuru Mungu baada ya kushiriki meza ya Bwana
watu waliofungwa na nguvu za giza wakiombewa maara baada ya kushiriki meza ya Bwana.

Kanisa la EAGT City Center limeweka mkakati wa kuwaleta watu elfu 9 kwa yesu katika kongamano la siku 90 ambapo limeanza rasmi Aprili tatu mwaka huu na linategemewa kuhitimishwa Julai tatu mwaka huu ndani ya kanisa hilo lilopo Mtoni Mtongaji jijini Dar es salaam.
Akizungumza katiuka uzinduzi wa wa kongamano hilo la siku 90 askofu na mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Askofu Florian katunzi alisema kuwa wamejipanga katika kuhakikisha kuwa katika siku zote hizo watu wanamrudia Bwana Yesu akma Bwana na mwokozi katika maisha yao na kufunguliwa kutokana na matatizo na shida mbalimbali.
Aidha alisema kuwa wale wote wanaaotaabika na kupitia katika mapito magumu ya ugonjwa biashara na hata katika familia zao wafiki na kumtafuta Mungu wa kweli ndani ya siku hizo tisini na kiukweli Mungu anashuka na kuwatembelea na kuwaweka huru mbali na mateso na maonevu ya Adui.
Aliongeza kuwa katika kongamano hilo la siku 90 watashirikiana na wahubiri wengine katika kuhakikisha kuwa waumini na wasiowaumini watakaofika watafunguliwa na kuinuliwa kutoka hatua moja kwenda nyingine ambapo alisema kuwa ataanza yeye  mchungaji na askofu Katunzi ,Mchungaji Atunus Kamili kutoka mbeya,mchungaji  Abudi Misholi kutoka mbeya ,mchungaji Joshua Wawa kutoka Sengerema na kulola Juounir( Michael) kutoka Mwanza.
Katika maombi haya kila mmoja ataenda kumwona Mungu katika maisha yake ya kila siku na katika sehemu yake ya kazi na  kuleta kibali katika maisha ya kila mmmoja katika kila jambo aingiapo na atokapo maana  Mungu anaenda kufanya Mbingu ikufungukie na kubarikiwa na kuwekwa huru katika maisha na majukumu ya kila siku na kwa kila unachokifanya Mungu anatenda mambo makuu.
"Ndani ya siku 90 inawezekana umekutana na mchungu na magumu ila katika siku hizo Mungu anaenda kuleta mageuzi na kuponya maisha yako, kazi yako, watoto wako nao watakuwa huru na kufunguliwa ambapo alinukuu kitabu 1samweli 22:1-2"alisema askofu Katunzi.
"inawezekana unauchungu na madeni na mpito magumu katika siku zako na maisha yako ya kila siku sasa katika siku zote 90 Mungu anaenda kuondoa uchungu na magumu unayopitia na kuwekwa huru maana   unateseka  katika maisha yako Mungu anaenda kukumbuka na kukutana na maisha matamu, ndoa nzuri, kazi safi hata kama ulidharauliwa Mungu anaenda kuleta mageuzi na kukurudishia heshima na mengi na maajabu mengi unaenda kukutana nayo''aliongeza askofu Katunzi.
Akisoma kitabu cha Ayoubu 15:25-26
Alisema kuwa Yesu ni mtetezi wa kila mwanadamu na hata kama umeonewa na kuteseka unaenda kufunguliwa haijalishi kuwa umekandamizwa na kuumizwa  Mungu anaeonekana na kukusaidia maana yeye anafahamu na kutambua  kesho na mwisho wako na kwake yeye inaenda kuwa mwisho  mwema.
Akiongeza kwa kufafanuzi zaidi na kunukuu kitabu cha Yeremia 33:3 alisema kuwa Mungu anasema kuwa umuuute naye anaenda kukuitikia hata kama watu wamekuona haufai wala hauna thamani mbele zao simama na Mungu mwite atakuonekania na kukuweka huru.

Hata hivyo alisema mapito unayopitia Mungu anaenda kuvusha  yale yanayokusibu ikiwa ni magonjwa,shida,taabu na mateso utawekwa huru na wale waliokuangusha wataanguka wao waliokuinamisha watainamishwa wao,na hata maadui zako wataenda kukatiliwa mbali nawe utapita bila kipingamizi.
Zaburi 1:1
Pia alisema kuwa inawezekana kuna watu walipanga unyauke usifaniukiwe ukwame kiuchumi sasa wao wanaenda kunyauka na kupotelea mbali maana Mungu wa kweli anaenda kukutana nawe hata kama ni magonjwa kama kansa, ukimwi na  magonjwa yote sugu yanaenda kunyauka kwa jina la Yesu na kuwekwa huru na kufunguliwa ndani ya siku 90.
"Waliokupiga wanaenda kupigwa ndani ya siku 90 waliokutesa na kukuinamisha kwa magonjwa wanaenda kuachia maana yupo mtetezi atake kukuinua katika haki utakuwa mbali katika kuonewa na kuteswa, wote waliokuwa kinyume nawe wataanguaka,walioweka mitego na kuuwekea uharibifu wanaaenda kuanguaka na kusambaratika mbele yako"alisema askofu Katunzi kwa masisitizo.

Kutokana na hayo alisema kuwa Hali ya umaskini inaenda kunyaushwa maana Mungu anasema yeye ni moto ulao na anaenda kukutembelea uliyefungwa na kuonewa na adui hata katika familia yako ambapo kila siku saa mbili jumamosi hadi saa nane ibada inaaza na kuhitimishwa na siku ya jumapili ibada inaanza saa 12 hadi tatu ibada ya kwanza na na ibada ya pili inaaza saa tatu hadi saa nane.

Sunday 10 April 2016

 Askofu Josephat Katunzi akifundisha neno la Mungu katika kanisa la EAGT City Center iliyopo Mtoni Mtongani.
 akifafanua neno ndani ya kanisa la EAGT.
 Pokea kwa jina la Yesu mtenda miujiza.
 Maombi na maombezi yakiendelea ndani ya kanisa hilo la EAGT City Center.


 Waliovamiwa na mapepo wakifunguliwa kwa jina la Yesu.
 pokea uponyaji kwa jina la Yesu.
 Zoezi la maombi na maombezi limeanza kwa jina la Yesu.

 Inua mikono juu kwa ajili ya kufunguliwa katika matatizo yako unayopitia .
Mtu mmoja mabye aliletwa akiwa hajiwezi na kuombewa na mtumishi wa Mungu askofu Katunzi.

Imeelezwa kuwa katika maisha ya waumini kuna vizuizi mbalimbali ambavyo vinasababisha muumini asifikie malengo yake  hasa kiroho na kimwili.

Kauli hiyo imetolewa na askofu wa jimbo la temeke na pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa la EAGT City Center  iliyopo  mtoni mtongani jijini dar es salaam.
Akifundisha somo la MAOMBI YA UKOMBOZI UFUNGUO WA sehemu ya 16 (PASAKA) ambayo ni KUFUFUKA NA KUHUISHWA,alisema kuwa kuna vizuizi ambavyo vinawakwamishwa watu katika maisha yao ya kila siku na vinaondolewa na nguvu za ufufuo ambayo Bwana Yesu ndiye anaweza tu kuwafungua.
Akinukuu kitabu cha  hosea 13:14 kunawatu wamefungwa katika maisha yao katika kazi nyumbani na hata katiika familia zao
Yohana 11:1-44
Yesu ndiyo ufufuo na uzima akiingia ndani ya maisha yako unawekwa huru katika maisha yako kazini kwako na hata katika chochote unayofanya.
inawezaka ulikuwa unaumwa umeteseka umepitia katika maisha magumu lakini mpaka sasa yesu anafufua kila kitu katika maisha yako maana yeyey ndiye ufufuo n uzima.
kuna mambo ambyo yameshindikana katika maisha ya mwanandamu ila kwa mungu yanawexzdekana maana muujiza hauwezi kuwa muujiza kama mwanadamu anaweza kuufanya katika maisha yake.
Hata hivyo alisema kuwa kuna watu wamefungwa na udini na udhehebu wake na bado Mungu anawahitaji kuwafungua katika maisha yao na ndiyo maana nimeamua kuanzisha ibada ya jumamosi.
ili kufanikiwa kuwa vuta wateja na kuwaweka katika maisha yao inatakiwa uweke mikakati na mbinu ya kuwavuuta ili waweza kuwepo katika kundi la kufunguliwa na kuwekwa huru katika maisha yao.
Kuna waumini wangi wanamalka ya kutumia ila hawajui jinsi ya kutumia mamlaka hiyo maana katika maisha ayako unaweza ukawa na elimu kumbe imekufa biashara kazi na hata ndoa imekufa sasa unamamlaka ya kuita katika maisha yako na kuitika na kufunguka katika maisha yako.
Bwana Yesu alipoenda kwa akina matha na Mariamu ambayo ndugu yao lazaro alikuwa yesu aliwaambia tu kuwa toeni jiwe na kuita lazaro toka nje naye akatoka sasa anawe unaweeza kuita  mambo yako na itaoka katika kundi ambalo uliwekwa.
kunawatu ambao walilaaniwa na shangazi na watu wao lakini kwa Mungu hayo yote yanawezekana nawewwe unatakiwa useme wakati ukishika sadaka yako ,maana Mungu amekupa neno la kusema ili kufufua mambo yako yaliyokufa NA kuwa huru.
Yesu alisema nitaweka roho yangu juu yao nayo inatwaweka watu wangu juu.

Total Pageviews

Eagt City Centre Blog 2013. Powered by Blogger.

About Me

My photo
Jicho langu latoka machozi lisokome,wala haliachi;Hata BWANA atakapoangalia. Nakutazama toka mbinguni Maombolezo 3:49-50

Followers

Featured Posts

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget