mchungaji Florian Katunzi akifundisha neno la Mungu ndani ya Kanisa la EAGT lilopo mtoni mtongani.
Mchungaji Florian katunzi akiwaombea baadhi ya watu waliodondoka wakati wa ibada ya maombezi ndani ya kanisa la EAGT City Center.
sasa ni wakati wa kila mmoja kuombewa na mchungaji katunzi ambapo watu mbalimbali walifika na kuanza kupita madhabahuni kuombewa
mchungaji Florian Katunzi wa EAGT City Center akiwa na mchungaji msaidizi Sospeter Mgema wakati wa kuanza ibada ya maombi na maombezi.
ni wakati wa maombi na maombezi sasa ni zamu ya kila mmoja kujiombea wakati ibada ya maombezi na maombi haijaanza.
Kila mmoja kujiombea ndani ya kanisa la EAGT chini ya mchungaji Florian Katunzi
Na Stelius Sane,
Imebainika kuwa asilimia kuwa ya
waumini wamekuwa wakipitia katika mapito magumu ya kukatisha tama na kushindwa
kuinuliwa na kufanikiwa kutokana na mafungo mbalimbali yaliyowafunga na
kuwafanya kushindwa kustawishwa.
Hayo yalisemwa na mchungaji kiongozi
wa kanisa la EAGT City Center lilopo mtoni mtongani jijini Dar es
salaam,mchungaji Florian Katunzi ambapo alisema kuwa kuna mafungo ambayo
imewakwamisha katika njia zao ya ustawisho.
Aidha mchungaji Katunzi alisema kuwa
katika taifa la Tanzania kuna makaburi ambayo ni kukosekana kwa mvua hakuna
kustawishwa wala kuinuliwa ila sasa Mungu anaende kutenda na kufufua kazi ya
mikono ya kila mtanzania ambaye atasimama katika nafasi yake na kumtafuta Mungu
wa kweli kwa bidii bila kujali kuwa umezikwa kwa muda gani.
Mchungaji katunzi aliongeza kuwa akaniambia tena, Toa
unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana. Bwana MUNGU
aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi
mtaishi.Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na
kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya
kuwa mimi ndimi Bwana.
Aidha aliendelea kunukuu na kusema kuwa Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe. Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake. Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi.
Aidha aliendelea kunukuu na kusema kuwa Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe. Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake. Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi.
Hata hivyo aliendelea kuwa Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa.Basi tabiri, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli.
Pamoja na hayo alifafanua kwa kunukuu kuwa Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu.Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimesema hayo, na kuyatimiza, asema Bwana.
Akifafanua kwa undani juu ya nguzo
hiyo ya pili ambayo ni imani alisema kuwa ni njia ya kupokea kutoka kwa Mungu
ambayo ni kule kumtumainia Mungu katika hali zote na kuishi katika neon maana
chanzo cha nguzo hii ni nguzo ya kwananza ambayo ni neno la Mungu.
Kuomba kwa imani inasababisha jambo
kutendeka kama vile neno linavyosema maana ukitumia nguzo hii unafanikiwa na
kuwa katika viwango vingine sawa na kitabu cha Waebrania 11:1-2 Basi imani ni
kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana,Maana
kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa.
Katika kitabu cha Ezekieli alipokuwa
akizungumzia mifupa mikafu ikimaanisha ni hali ya ukame ambayo inaweza kuwa ni
ukame katika huduma yako,elimu yako,maisha yako na pia inawezekana ni ukame
katika kila unachofanya kwa mikono yako.
Kutabiri ikiashiria ni kuomba kwa
imani juu ya hali yako unayopitia na kusababisha kukata tamaa na kuona kama
haiwezekani sasa ni wakati wako kusimama na kutabiria maisha yako ili ufanikiwa
na kuinuliwa katika kila jambo unalofanya
Mchungaji katunzi akinukuu kitabu cha Warumi 10:17 alisema kuwa Basi imani,
chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.
Katika maisha ya kina mwanadamu
inawezekana kuna vitu vimekukandamiza na kukumiza na kukufanya ushindwe
kufanikiwa sasa ni zamu ya kuinuliwa bila kujali walikuzika na kukufunga kwa
njia gani.
“Yakobo 1:22 inasema kuwa Lakini iweni watendaji wa neno, wala
si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu”alinukuu mchungaji katunzi
Aliongeza kuwa kuna baadhi ya watu
wanasikiliza neno la Mungu lakini hawalifanyii kazi badala yake wanabaki tu
maana cha cha imani ni kusikia,neno la Mungu na ukiwa msikiaji na hutendei kazi
matokeo yake unabaki kudumaa katika maisha.
Inawezekana umezikwa katika makaburi
ya babu zenu na ukoo zetu kwa kuchukua nywele na kucha zenu na kuzika
unaonekakna unaishi lakini maisha yako yamezikwa katika makaburi sasa ni wakati
wa kuwekwa huru.
Hata kama umezikwa kiasi kwamba hata
huwezi kufanikiwa katika kila unachokifanya Mungu wa kweli kwa jina la Yesu
unafunguliwa hata kama wamekupa majina kutokana na tatizo unalopitia unawekwa
huru na kufanikiwa .
“Katika taifa la Tanzania kuna
makaburi ambayo ni kukosekana kwa mvua hakuna kustawishwa wala kuinuliwa ila
sasa Mungu anaende kutenda na kufufua kazi ya mikono ya kila mtanzania ambaye
atasimama katika nafasi yake na kumtafuta Mungu wa kweli kwa bidii bila kujali
kuwa umezikwa kwa muda gani”alisema mchungaji katunzi.
Katika taifa kama ikikosekana Mvua
ama mafanikio biblia inasema kuwa waumini waliomtambua Bwana Yesu kama mwokozi
wa maisha yao kuomba kwa bidii na Mungu anatenda maana yeye anatenda anyefahamu
maisha ya kila mwanadamu.
Akinukuu kitabu cha Zekaria
10:1 inasema kuwa Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam,
Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi
kondeni.
“Ni wakati wako kusimama na kumwomba
Mungu alete mafanikio na kleta mvua ya Baraka itakayoleta ustawisho na
mafanikio na sio mvua zenye madhara”, alisema mchungaji Katunzi.
Ni wakati wa kusimama na kutenda kwa
imani maana ni nguzoo ya pili ya urejesho itakayokusaidia kutekeleza na
kufanikiwa kiuchumi na katika kazi ya mikono yako.
Msomaji unaweza
kufuatilia kipindi cha saa ya ushindi na kufunguliwa kupitia runinga ya chanel
Tena kuanzia saa mbili na nusu usiku na kurudiwa jumatano saa kumi na moja
jioni na kusikiliza wapo redio kila jumapili saa nne kamili hadi saa tano na
kurudiwa jumatatu saa sita mchana
Ama tembelea
pastorkatunzi.blogspot.com
Kwa mawasiliano
0784367826,0754367826
Na 0718267171
0 comments:
Post a Comment