Thursday 28 May 2015

SILAHA NANE ZA KUFUNGUA MILANGO NA MALANGO YALIYOFUNGWA MBELE YAKO;

SILAHA YA NNE 

INUKA KWA IMANI
Malango ya Israeli yalifungwa muda wa miaka ishirini, Mashujaa walikoma, Watu walionewa kwa nguvu za Sisera muda wa miaka ishirini, lakini Sisera alikomeshwa na mwanamke wa Imani Debora aliyeinuka akaongoza vita dhidi ya Sisera Wana wa Israeli wakamlilia BWANA; kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma mia kenda, naye akawaonea wana wa Israeli kwa nguvu muda wa miaka ishirini. Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi, siku za Yaeli, njia kuu zilikuwa hazina watu; Nao wenye kusafiri walipita kwa njia za kando. Maliwali walikoma katika Israel, walikoma, Hata mimi Debora nilipoinuka, Nilipoinuka mimi, mama katika Israeli.
hakika kwa mkono wa BWANA Sisera alianguka. Maandiko matakatifu yanathibitisha waziwazi na kusema;

“Hata alipokufa Ehudi wana wa Israeli wakafanya yaliyo maovu tena mbele za macho ya Bwana. Bwana akawauza na kuwatia katika mkono wa Yabin Mfalme wa Kaanani aliyetawala huko Hazori na sisera aliyekaa katika harosheth wa mataifa, alikuwa amiri wa jeshi lake. Wana wa Israel wakamlilia Bwana kwakuwa sisera alikuwa na magari ya chuma mia kenda, naye akawaonea wana wa Israeli kwa nguvu muda miaka ishirini. Basi Debora nabii mke mkwewe Lapidoth ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule. Naye alikaa chini ya mtende wa Debora kati ya Rama na Bethel katika nchi ya vilima vilima ya Efreaim, Wana wa Israeli wakakwea kwake awaamue. Huyo akatuma mtu akamwita Baraka wa Abinoam toka Kedeshi naftari akamwambia je! Bwana Mungu wa Israel hakutoa amri? Akisema enenda ukawavute kwako huko katika mlima wa Tabora, watu elfu kumi wa wana wa Naftari na wana wa Zabron. Nami nitakuvutia Sisera amiri wa jeshi lake Yabin hata mto wa kishon pamoja na magari yake na wingi wa watu wake nami nitamtia mkononi mwako. Baraka akamwambia, kama utakwenda pamoja nami ndipo nitakwenda bali kama huendi pamoja nami, mimi siendi. Basi akasema, hakika nitakwenda pamoja nawe lakini safari utakayoiendea haitakupatia heshima wewe maana Bwana atamuuza Sisera katika mkono wa mwanamke Debora, akainuka akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedesh. Baraka akawakutanisha Ftari na Zabron waende Kedesh wakakwea watu elfu kumi wakimfuata Debora, naye akaenda pamoja naye. Basi heberi, mkeni alikua amejitenga na wake yaani na wana wa Hobab Shemeji yake Musa, akaipiga hema yake mbali penye mualoni uliopo saa na imu karibu na Kedesh. Watu wakamwambia Sisera yakwamba Baraka mwana wa Abinoam amekwea kwenda mlima wa Tabora. Sisera akayakusanya magari yake yote, naam magari ya chuma ni ya kenda na watu wote waliokuwa pamoja naye toka herosheth wamataifa mpaka mto wa kishon. Debora akamwambia Baraka, haya? Inuka maana siku hii ndiyo siku ambayo Bwana amemtia Sisera katika mkono wako, Je! Bwana hakutoka atangukie mbele yako? Basi Baraka akashuka katika mlima wa Tabora na watu elfu kumi wakamfuata. Bwana akamfadhaisha Sisera na magari yake yote, na jeshi lake lote, kwa makali ya upanga, mbele ya Baraka; basi Sisera akashuka katika gari lake, akakimbiakwa miguu. Lakini Baraka akayafuatia magari, na jeshi, hata Haroshethi wa Mataifa, na hilo jeshi lote la Sisera likaanguka kwa makali ya upanga; hakusalia hata mtu mmoja.lakini Sisera akakimbia kwa miguu, akaifikilia hema ya Yaeli mkewe Heberi, Mkeni; kwa maana palikuwa na amani kati ya Yabini, mfalme wa Hazori, na nyumba ya Heberi, Mkeni. Yaeli akatoka kwenda kumlaki Sisera, akamwambia, Karibu Bwana wangu, usiogope. Akakaribia
kwake hemani, naye akamfunika kwa bushuti. Akamwambia, Tafadhali nipe maji kidogo ninywe; maana nina kiu, Akafungua chupa ya maziwa, akampa kunywa, akamfunika. Naye akamwambia, Simama mlangoni pa hema; kasha itakuwa mtu awaye yeyote akija na kukuuliza, akisema, Je! Yupo mtu hapa, basi, mjibu, La, hapana. Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akashika nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akamtia kile kigingi katika kipaji chake, nacho kikapenya, hata kuingia mchangani; kwa maana usingizi mzito ulikuwa umemshika, basi akazimia, akafa. Na tazama, Baraka alipokuwa akimfuatia Sisera; Yaeli akatoka ili kumlaki, akamwambia, Njoo, nami nitakuonyesha yule mtu unayemfuata. Basi akamwendea, na tazama, Sisera amelala humo, amekufa, na hicho kigingi kilikuwa kipajini mwake. Basi hivyo Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani mbele ya wana wa Israeli siku hiyo. Mkono wa wana wa Israeli ukazidi kupata nguvu juu ya Yabini, mfalme wa Kanaani, hata walipokuwa wamemuangamiza Yabini, mfalme wa Kanaani.” Waamuzi 4:1-24

“Debora akamwambia Baraka, Haya! Inuka;  maana siku hii ndiyo siku ambayo BWANA amemtia Sisera katika mkono wako. Je! BWANA hakutoka atangulie mbele yako? Basi Baraka akashuka katika mlima wa Tabora, na mtu elfu kumi wakamfuata.” Waamuzi 4:14

Malango na milango itakufungukia pale utakapoinuka kwa silaha ya imani “ KUINUKA KWA IMANI.” Neno Inuka  lina maana kubwa sana, angalia miaka nenda rudi Mwanamke huyu amekuwa tasa na kila mwaka alikwenda Hekaluni kusali na kutoa sadaka mbele za Mungu aliye hai lakini aliendelea kuwa tasa, mlango wake wa uzazi ulifungwa. Wako watu watu wengi wanasali, wanatoa sadaka lakini Malango na Milango imefungwa mpaka wachukue hatua ya “Kuinuka wenyewe wa imani” Hana akainuka toka kwenye Utasa na Ugumba, akamwendea BWANA kwa Maombi mazito. Yenye kufungua milango na malango, na alipoinuka alikutana na BWANA, hakika ukawa ndio mwisho wa huzuni zake. Tunasoma maandiko yanasema; “Palikuwa na mtu mmoja wa Rama, Msufi, wa nchi ya milima milima ya Efraimu, jina lake akiitwa Elkana, mwana wa yerohamu, mwana wa Sufu, Mwefraimu, naye alikuwa na wake wawili, jina lake mmoja akiitwa Hana, na jina lake wa pili aliitwa Penina, naye huyo Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto. Na mtu huyo alikuwa akikwea kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea BWANA wa majeshi dhabihu katika Shilo, Na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, makuhani wa BWANA, walikuwako huko. Hata siku ile ilipofika Elkana alipotoa dhabihu, kumpa mkewe Penina sehemu, akawapa na watoto wake wote, waume kwa wake, sehemu zao; lakini Hana humpa sehemu mara mbili; maana alimpenda hana, ingawa BWANA alikuwa amemfunga tumbo. Ila mwenzake humchokoza sana, hata kumsikitisha, kwa sababu BWANA alikuwa amemfunga tumbo. Tena mumewe akafanya hivyo mwaka kwa mwaka, hapo yule mwanamke alipokwea kwenda nyumbani kwa BWANA, ndivyo yule alivyomchokoza; basi, kwa hiyo, yeye akalia, asile chakula. Elkana mumewe akamwambia, Hana, unalilia nini? Kwani huli chakula? Kwa nini moyo una huzuni? Je! Mimi si bora kwako kuliko watoto kumi? Ndipo Hana akainuka, walipokwisha kula na kunywa huko Shilo. Naye Eli, kuhani, alikuwa akiketi kitini pake penye mwimo wa hekalu la BWANA. Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamwomba BWANA wa majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapompa BWANA huyo mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautamfikilia kichwani kamwe. Ikawa, hapo alipodumu kuomba mbele za BWANA, Eli akamwangalia kinywa chake. Basi Hana alikuwa akinena moyoni mwake; midomo yake tu ilionekana kama anena, sauti yake isisikiwe; kwa hiyo eli alimdhania kuwa amelewa. Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini? Achilia mbali divai yako. Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana. Usimdhanie mjakazi wako kuwa ni mwanamke asiyefaa kitu; kwa kuwa katika wingi wa kuugua kwangu na kusikitika kwangu ndivyo nilivyonena hata sasa. Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu wa Israeli akujalie haja yako uliyomwomba. Naye akasema, Mjakazi wako na aone kibali machoni pako. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake haukukunjamana tena. Wakaondoka asubuhi na mapema, wakasali mbele za BWANA, kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye BWANA akamkumbuka. Ikawa wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, kwa kuwa Nimemwomba kwa BWANA. Kisha yule mtu, Elkana, na watu wote wa nyumbani mwake, wakakwea kwenda kumtolea BWANA dhabihu ya mwaka, na nadhiri yake. Bali Hana hakukwea; maana alimwambia mumewe, Sitakwea mimi hata mtoto wangu atakapoachishwa maziwa, hapo ndipo nitakapomleta, ili ahudhurie mbele za BWANA, akae huko daima. Elkana, mumewe, akamwambia, Haya, fanya uonavyo vema; ngoja hata utakapomwachisha maziwa; BWANA na alithibitishe neno lake tu. Basi yule mwanamke akangoja, akamnyonyesha mtoto wake, hata akamwachisha maziwa. Naye alipokuwa amekwisha kumwachisha maziwa, akamchukua pamoja naye, na ng’ombe watatu, na efa moja ya unga, na chupa ya divai, akamleta nyumbani kwa BWANA, huko Shilo; na yule mtoto alikuwa mtoto mdogo. Nao wakamchinja huyo ng’ombe, wakamleta mtoto kwa Eli. Akasema Ee bwana wangu, kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mimi ndimi yule mwanamke aliyesimama karibu nawe hapa, nikimwomba BWANA. Naliomba nipewe mtoto huyu; BWANA akanipa dua yangu niliyomwomba; kwa sababu hiyo mimi name nimempa BWANA mtoto huyu; wakati wote atakaokuwa hai amepewa BWANA. Naye akamwabudu BWANA huko.” 1Samweli  1:1-28

Ikawa hapo alipoendelea kuomba mbele za BWANA, Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamuomba BWANA akalia sana. Kuhani Heri akamwendea na kumtamkia neno la kumfungua tumbo lake, naye akaenda nyumbani mwake, majira yalipotimia akampata mtoto akamwita Samweli. Lazima uchukue hatua ya Kuinuka kuyaendea Malango na Milango iliyofungwa mbele yako nayo itafunguka. Maana kila hatua unayoipitia na kila hatua unayoichukuwa, BWANA ataifanikisha. Mtu wa Mungu usipoinuka utabaki vivyo hivyo japo umeokoka. Kwa Imani lazima Uinuke umwendee Mungu naye atafanya njia mbele yako ambayo wewe kwa macho ya kawaida huioni. Angalia watu hawa wanne wenye ukoma, walichukua hatua ya KUINUKA KWA IMANI, na Mungu akawasikizisha mbele ya maadui zao wakawa lango la ukombozi kwa taifa zima la Israeli. Neno la Mungu linasema; “Basi walikuwapo watu wanne wenye ukoma, penye lango la mji, wakasemezana, mbona tunakaa hapa hata tufe? Tukisema, tutaingia mjini, mjini mna njaa, nasdi tutakufa humo, nasi tukikaa hapa, tutakufa vile vile. Haya twende tukaliendee jeshi la Washami, wakituhifadhi hai tutishi, wakituua tutakufa tu. Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami, na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu. Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa, wakaambiana, tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi. Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao. Basi wale wenye ukoma walipofika mwisho wa kituo, waliingia katika hema moja, wakala na kunywa, wakachukua fedha, na dhahabu na mavazi,  wakaenda wakavificha, wakarudi, wakaingia katika hema ya pili, vile vile wakachukua vitu, wakaenda wakavificha. Ndipo wakaambiana, mambo haya tufanyayo si mema, leo ni siku ya habari njema nasisi tunanyamaza, tukingoja hata kutakapopambazuka, madhara yatatupata, basdi twende tukawaambie watu wa nyumba ya mfalme. Basi wakaenda, wakawaita mabawabu wa mji, wakawaambia, tulifika kituo cha Washami, na tazama hapana mtu yeyote huko, wala sauti ya mtu ila farasi wamefungwa, na punda wamefungwa na hema zao kama walivyoziacha. Na mabawabu wakawaambia watu wa nyumba ya mfalme. Mfalme akaondoka usiku, akawaambia watumishi wake, sasa nitawaonyesha ninyi walivyotutendea Washami. Wanajua yakuwa tuna njaa, basi wametoka kituoni ili kujificha kondeni, wakisema watakapotoka mjini, tutawakamata hai, tena tutapata kuingia mjini, na mmoja wapo wa watumishi wake akajibu, akasema, kunradhi, baadhi ya watu na watwae farasi watano katika hao waliosalia, waliobaki ndani ya mji (tazama wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli waliobaki ndani yake; tazama wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli walioangamia), tukawapeleka tukaone. Basi wakatwaa magari mawili na farasi zake, mfalme akawatuma kuwafuata Washami, akasema, Enendeni, mkaangalie. Wakawafuata mpaka Yordani na kumbe! Njia yote ilikuwa imejaa mavazi  na vyombo, walivyovitupaWashami, wapate kukimbia upesi. Watu wale waliotumwa wakarudi, wakamwambia mfalme, basi watu wakatoka, wakaziteka nyara hema za Washami. Ikawa kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekel, sawasawa na nenola BWANA. Naye mfalme akamweka yule akida, ambaye alitegemea mkono wa ke, awasimamie watu langoni; na watu wakamkanyaga langoni, akafa, kama alivyosema yule mtu wa Mungu, aliyenena hapo mfalme alipomshukia.ikatukia kama vile yule mtu wa Mungu alivyomwambia mfalme, vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, na kipimo cha unga mzuri kwa shekeli ndivyo vitakavyokuwa kesho, panapo saa hii, katika lango la Samaria, na yule akida akamjibu mtu wa Mungu akasema, sasa tazama kama BWANA angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akasema, angalia wewe utaliona kwa macho yako lakini hutakula.” 2 Wafalme  7:3-19

Watu hawa walitupwa nje ya lango la mji wafe na njaa. “Wakaasemezana wao kwa wao; mbona tunakaa hapa hata tufe?” Ili wasife ni lazima wachukue hatua ya KUINUKA KIIMANI kutoka kwenye “Kifo” Kwa sababu kwenye lango la Samaria mpaka ndani ya mji wa Samaria kulikuwamo vifo vilivyotokana na njaa kali kiasi cha watu walikula watoto wao. Nje ya Samaria kulikuwa na chakula, lakini kilikuwa mikononi mwa maadaui wa wana wa Israeli. Ndipo wakoma hawa wakachukua hatua ya kukiendea kituo cha Washami kwa Imani, wakainuka wakasema; “Haya twende tukaliendee jeshi la Washami, wakituhifadhi hai, tutaishi na wakituua, tutakufa tuu.”

Wakainuka kwa Imani kungali bado mapambazuko ili waende mpaka kituo cha Washami, lakini walipofika mwanzo wa kituo cha Washami kumbe hamna mtu, Maadui wamekimbia mbele ya watu wenye Ukoma, walioamua KUINUKA KWA IMANI. Angalia Mungu anapenda mtu anayechukua hatua ya “KUINUKA KWA IMANI.”
Washami walikimbia kwasababu; BWANA alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari na kishindo cha farasi kama kishindo cha jeshi kubwa, Wakaambiana, tazama mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti na wafalme wa Wamori waje wapigane nasi. “Kishindo” cha Mungu, lazima kiambatane na mtu aliyekubali kuinuka kwa Imani. Nasi tukikubali kuinuka kwa Imani, kipo kishindo cha Mungu aliye hai, kitawakimbiza maadui zetu wataacha Malango yetu na Malango ya Baraka yakitufungukia.
Lazima kuinuka Kimaombi ndipo utasonga mbele, naye Mungu atakushika mkono wako na kukuinua. “Bwana huzikomboa nafsi za watumishi wake, Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao.” Zaburi 34:22

Tunapoendelea kuinuka kwa Imani tunayafungua Malango na milango. “Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, akamuokoa na taabu zake zote. Malaika wa BWANA hufanya kituo pale aketipo, akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.” Zaburi 34:6-7

Kuinuka na Kumwita Mungu kunafungua Malango. Huu ni wakati wa Kuinuka tena Kiimani. Na kushika kazi za mikono ili tupate kumilikishwa katika BWANA, ndiyo maana BWANA anatoa wito wa kuinuka na kushika kazi sawasawa na neno lake; “Ya dhahabu, ya fedha, naya shaba naya chuma, hapana hesabu, basi inuka ushike kazi, naye BWANA na awe pamoja nawe.” 1Mambo ya Nyakati 22:16

Mungu anatafuta mtu atakayeinuka na kusimama mbele zake ili kuyafungua Malango na Milango iliyofungwa. Naye BWANA atageuza ishara za waongo na wachawi zisitende kazi. Maandiko matakatifu yabasema; “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.” Ezekieli 22:30

Yatupasa kuinua watoto wetu, ndoa zetu, biashara zetu, maisha yatu kwa ujumla mbele za Mungu aliye hai. Maana hayo mateso hayatainuka tena mara ya pili. Inua Misingi yako ya uchumi iliyobomoka. Pembe ya mwenye haki  itainuka daima pale atakapoiinua ndani mwa maombi. Maandiko yanasema; “Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Naam, viinueni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia.” Zaburi  24:9

Usikubali nafsi yako kuinama kwa huzuni, bali Inuka uyafungue Malango yako nayo yatafunguliwa. “Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.” Zaburi  75:10

Daudi, anaomba anasema; “Amka, utukufu wangu. Amka, kinanda na kinubi, nitaamka alfajiri.” Zaburi  57:8
Vita vyote unavyopitia, utavishinda pale utakapochukua hatua ya Imani ya kuyaendea malango ya adui katika Maombi na kuyafisha.
Na waangamie vivyo maadui zako, kama Sisera alivyoangamia mbele ya BWANA. Kwa mkono wa Debora, mateso yalikomeshwa dhidi ya Israeli. Kwa muda wa miaka arobaini, Israeli alistareheshhwa na BWANA. Heshima ya Israeli ilirejea tena kwa Imani walipokubali kuinuka.











0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

Eagt City Centre Blog 2013. Powered by Blogger.

About Me

My photo
Jicho langu latoka machozi lisokome,wala haliachi;Hata BWANA atakapoangalia. Nakutazama toka mbinguni Maombolezo 3:49-50

Followers

Featured Posts

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget