Thursday 28 May 2015

SILAHA NANE ZA KUFUNGUA MILANGO NA MALANGO YALIYOFUNGWA MBELE YAKO;

SILAHA YA TANO

REJESHA KILA KILICHOKUWA KIMECHUKULIWA;

Katika hatua hii ya tano, ni hatua ya urejesho maana baada ya kuokolewa Kristo Yesu amekusudia kuturejeshea Baraka na Ustawi. Maandiko matakatifu yanathibitisha kwa kinywa cha nabii Isaya;  “BWANA akapendezwa, kwaajili ya haki yake, kuitukuza sheria, na kuiadhimisha. Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa, wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza, wamekuwa mawindo wala hapana aokoaye, wamekuwa mateka wala hapana asemaye rudisha. Ni nani miongoni mwenu atakaye tega sikio lake kuyasikia hayo? Atakayesikiliza na kusikia kwa wakati ujao? Ni nani aliyemtoa Yakobo awe mateka, aliyemtia Israeli katika mikono ya wanyang’anyi? Si yeye, BWANA? Yeye tuliyemkosa, ambaye hakutaka kwenda katika njia zake, wala hawakuitii sheria yake.” Isaya 42:21-25

BWANA anasema wazi wazi yakuwa wako watu walioibiwa Baraka zao na ustawi, wengine wameibiwa ufaulu na uelewa wao katika masomo,wengine wameibiwa uchumi na utajiri wao, wengine wameibiwa ndoa zao na mengine mengi yanayofanana na haya. Lazima tusimame ndani mwa maombi  na kurejesha kila kilichoibiwa na adui shetani. Maombi ugeuza hali pale watu wa Mungu wanapoomba kwa nia moja na moyo mmoja, hakika Mungu atafungua. Tunajifunza kwa wana wa Israeli kipindi cha nabii Samweli jinsi walivyoinuka, wakamlilia BWANA naye akawaitikia. Nakuwafadhaisha maadui zao. Maandiko yanathibitisha katika kitabu cha Samweli; “Samweli akasema, Wakusanyeni Israel wote Mispa, name nitawaombea ninyi kwa BWANA. Wakakusanyika huko Mispa, wakateka maji na kuyamimina mbele za BWANA; wakafunga siku ile, wakasema huko, tumemfanyia BWANA dhambi. Samweli akawaamua wana wa Israeli huko Mispa. Hata Wafilisti waliposikia ya kuwa wana wa Israeli wamekusanyika huko Mispa, mashehe wa Wafilisti walipanda juu ili kupigana na Israeli. Nao wana wa Israeli waliposikia, wakawaogopa Wafilisti. Wana wa Israeli wakamwambia Samweli, Usiache kumlilia BWANA, Mungu wetu kwa ajili yetu, kwamba atuokoe na mikono ya Wafilisti. Ndipo Samweli akatwaa mwana-kondoo mchanga, akamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa nzima, Samweli akamlilia BWANA kwa ajili ya Israeli, BWANA akamwitikia. Hata Samweli alipokuwa akiitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakakaribia ili kupigana na Israeli; walakini BWANA akapiga ngurumo, mshindo mkubwa sana, juu ya Wafilisti siku ile, akawafadhaisha, nao wakaangamizwa mbele ya Israeli. Nao watu wa Israeli wakatoka Mispa, wakawafuatia Wafilisti, wakawapiga hat walipofika chini  ya Beth-kari. Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akasema, Hata sasa BWANA ametusaidia.hivyo Wafilisti walishindwa, wasiingie tena ndani ya mipaka ya Israeli; na mkono wa BWNA ulikuwa juu ya Wafilisti siku zote za Samweli. Nayo miji ile Wafilisti waliyokuwa wamewapokonya Waisraeli ilirudishwa tena kwa Israeli, tokea Ekroni mpaka Gathi, na Waisraeliwakaukoa mpaka wake mikononi mwa Wafilisti. Tena kulikuwa na amani kati ya Israeli na Waamori. Naye huyo Samweli akawaamua Israeli siku zote za maisha yake.” 1 Samweli  7:5-14

Israeli chini ya Nabii Samweli, BWANA aliwashindia vita katika kusanyiko la Maombi ya kufunga. Maana wakati Samweli anatoa sadaka na dhabihu ya jioni madhabahuni pa BWANA; ikapigwa ngurumo na mshindo mkuu toka kwa BWANA ambao uliwafadhaisha Wafilisti ndipo Israeli wakashinda vita, baada ya kushinda ndipo wakarejesha yote yaliyokuwa yametekwa na Wafilisti. Nasi ndani mwa Maombi haya lazima turejeshe kila kilichochukuliwa na adui. Kama ni afya yako sharti uombe kwa Imani ukirejesha. Maana BWANA anasema, nitakurudishia afya, nitakuponya jeraha zako… Hata kama umeumwa sana lazima Uombe urejeshewe afya yako. “Naye atakurejezea uhai wako, na kukuangalia katika uzee wako, kwa maana mkweo ambaye akupenda, naye anakufaa kuliko watoto saba, ndiye aliyemzaa.” Ruthu  4:15

BWANA kabla ya kuwaokoa wana Israeli toka utumwani Misri, alipiga miungu ya Farao kwa mapigo kumi lakini kabla ya pigo ya mwisho, alimwambia Musa awaambie wana wa Israeli watake mali, toka kwa Wamisri naye BWANA atashusha nguvu ya kuwafanya Wamisri warejeshe mali mengi na utajiri kwa wana wa Israeli. “Basi nena wewe masikioni mwa watu hawa, na kila mtu mume na atake kwa jirani yake, na kila mwanamke atake kwa jirani yake, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu.” Kutoka  11:2

Malango ya Uchumi yatafunguliwa pale tu Mwombaji sharti kwanza atake mbele za Mungu kwa Imani. Lipo sikio linalosikia Maombi, Lazima Mali zilizofichwa na adui gizani, tuzitoe na turejeshe katika milki yetu.“Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata mapingo ya chuma; nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli.” Isaya  45:2-3

BWANA anasema atakufungulia Malango na Milango mbele yako, naye atakupa hazina, utajiri usio pimika, wewe na uzao wako maana wote walio kuonea watafadhaishwa naam wametahayarika mbele yako. Chukua hatua ya kuamini, Mali zako, Utajiri wako uje mikononi mwako maana Mungu aliyeziumba Mbingu na Nchi, yeye ndiye Mungu wako ataufanya Imara Uchumi wako, Hakutakuwa tena ndani mwako kufa-kufa na kuzaa mapooza.“kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.” Isaya  45:23

Ayubu anasema nimeomba BWANA, amesikia, nimemlilia yeye kwa sababu hiyo Mungu atamfanya mjane na yatima wabarikiwe na wataimba nyimbo za furaha badala ya maombolezo. Usiogope, Lango lako limefunguliwa, Rejesha Ustawi wako. Usikae kimya, Omba urejesho kwa nguvu. Mtumishi wa Mungu Ayubu, anaomba Mungu baada ya kufilisika, hana kitu, lakini anaomba tena Ustawi wa Mali zake.“Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia; Na jicho liliponiona, likanishuhudia. Kwa sababu nalimuokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia. Baraka yake yeye aliyekuwa karibu na kupotea ilinijia, nikaufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.” Ayubu  29:11-13
Lazima Mali zetu zitapikwe na wachawi walio tumeza lazima tuwakanyage matumbo yao kwa nguvu, tuwatapishe UTAJIRI wetu na HESHIMA. Baada ya Maombi haya, tutang’aa kama dhahabu mbele ya maadui zetu; maana BWANA anaugeuza uteka wako kuwa Baraka na Ustawi; ustawishwe na Uinuliwe na Urejeshewe Heshima. “Utukufu wangu utakuwa mpya, Na uta wangu hurejezwa upya mkononi mwangu.” Ayubu  29:20

Yeye aliyemeza mali ataitapika, maana BWANA ataitoa tumboni mwake. “Amemeza mali, naye atayatapika tena; Mungu atayatoa tumboni mwake.” Ayubu 20:15

HESHIMA AU CHEO

Esta  3:13-15
“Barua zikapelekwa kwa mikono ya matarishi mpaka majimbo yote ya mfalme kuwaangamiza Wayahudi wote, na kuwaua, na kuwafisha, vijana kwa wazee, watoto wachanga na wanawake pia, siku moja yaani siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili ndio mwezi wa Adari, na kuyachukuamali yao kuwa nyara. Nakili ya andiko, ya kupigwa mbiu katika kila jimbo, ilitangazwa kwa mataifa yote wawe tayari siku ile ile. Matarishi wakaondoka wakaenda haraka kwa amri ya mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. Mfalme na Hamani wakaketi ili kunywa divai, bali mji wa Shushani ukafadhaika.”

Esta na Modekai wanachukua hatua ya Kufunga na Kuomba. wakachukua hatua ya kuifuata Heshima yao kwa mfalme Ausuwelo. Esta akaingia kwa mfalme, ndipo Heshima ya Wayahudi ikarejeshwa, Aibu zao, Huzuni zao zikatenguliwa. “Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, name na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kasha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia na niangamie.” Esta 4:16

Ombea Uzao wako

“Basi ilikuwa, hapo hizo siku za karamu zao zilipokuwa zimetimia, Ayubu hutuma kwao akawatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na kusongeza sadaka za kuteketezwa kama hesabu yao wote ilivyokuwa; kwani Ayubu alisema, Yumkini kwamba hawa wanangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu moyoni mwao. Ndivyo alivyofanya Ayubu siku zote.” Ayubu  1:5

Esta; alisimama na kweli, Mungu akatenda



0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

Eagt City Centre Blog 2013. Powered by Blogger.

About Me

My photo
Jicho langu latoka machozi lisokome,wala haliachi;Hata BWANA atakapoangalia. Nakutazama toka mbinguni Maombolezo 3:49-50

Followers

Featured Posts

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget