Monday 22 August 2016































Imeelezwa kuwa katika kongamano la siku tisini watu mbalimbali waliokuwa na matatizo na shida mbalimbali wamefunguliwa na kuwekwa huru na wengi wameshuhudia jinsi Mungu alivyo wafungua katika taabu zao.
Akifundisha katika kongamano hilo mchungaji kiongozi wa kanisa la EAGT City Center Mchungaji Florian Katunzi alisema kuwa katika kongamano hilo kuna maombi ndani mwa maombi ambao  kuna vipengele mbalimbali na kwa wiki hiii inahitimika na kiengele cha kumiliki na kutawala.
Aidha alisema kuwa kuna baadhi ya watu wanamilikuwa na matatizoa mbalimbali kama vile magonjwa shida elimu jambo ambalo linawasasbabisha kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kila sai maana wamefungwa na kuwa chini ya vifungo hivyo.
Akinukuu kitabu cha  Isaya 26:11-14  ambapo alisema Bwana, mkono wako umeinuliwa, lakini hawaoni; lakini watauona wivu wako kwa ajili ya watu wako, nao watatahayari; naam, moto utawala adui zako. Bwana, utatuamuria amani; maana ni wewe pia uliyetutendea kazi zetu zote. Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametumiliki; lakini kwa msaada wako peke yako tutalitaja jina lako. Wao wamekufa, hawataishi; wamekwisha kufariki, hawatafufuka; kwa sababu hiyo umewajilia, na kuwaangamiza, na kuupoteza ukumbusho wao. 
Alisema kuwa kama vile wana wa israeli walivyokuwa wakimilikiwa na farao siku ya kutoka alipigwa kwa mapigo kumi na kuachia sasa na sasa kuna watu wanamilikiwa na umaskini ,roho za ukahaba, roho za kutokuolewa, kutokuoa na pia kuna roho za ushoga na usagali na ukiangalia utayaona kuwa hata katika ukoo wao kulikuwepo na tatizo kama hilo ndani ya ukoo wao.
"maombi ndani mwa maombi itakuwa ni maombi ambayo watu wataenda kukomesha matatizo na shida mbalimbali ambazo zilikuwa zinakukabili na kukutesa,maana wale wote waliokutesa kukuonea na kukutesa hwataishi",alisema mchungaji Katunzi.
Zaburi 107:13-14
ukishaokolewa na kuokoka na kuacha dhambi sasa unahamishwa na kuanza kumilikishwa katika maisha yako na utakuwa ukitawala katika maisha yako na hautateseka tena  na alinukuu kitabu cha warumi 5:17  Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. 
Alisema kuwa huwezi kumiliki kama Bwana Yesu hayupo ndani ya maisha yako inatakiwa kusimama kataika yeye na kumtegemea maana ndiye mwenye uwezo wa kukupa mamlaka ya kuondoa matatizo na kukemea mapepo na matatizo mbali mbali na yanaondoka.
Baada ya maombi haya ya kongamano  watu wengi wataanza kukushangaa na wengine watashangaa kukuona kuwa unaenda kuinuliwa na kuacha umaskini katika maisha yako yote maana pale utakapookoka Mungu anaenda kukubariki na kukufanikisha katika maisha yako na utakuwa mfano katika maisha yako.
ukisoma kitabu cha kutoka 11:1-3 inasema Bwana akamwambia Musa, Liko pigo moja bado, nitakaloleta juu ya Farao na juu ya Misri; baadaye atawapa ninyi ruhusa mtoke huku; naye hapo atakapowapa ruhusa, atawafukuza mtoke huku kabisa kabisa.  Basi nena wewe masikioni mwa watu hawa, na kila mtu mume na atake kwa jirani yake, na kila mwanamke atake kwa jirani yake, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu.  Bwana akawapa watu hao kibali machoni pa Wamisri. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake. 
Hata hivyo  aameongeza kuwa inachotakiwa ni kuhakikisha unafuata taratizi za Mungu na pia inatakiwa ujifunze juu ya suala la uchumi katika maisha yako unapoendelea na maombi na maombezi ili ufanikiwe na kufanikiwa.
Kanisa la eagt City Center limeanza kongamano la la siku tisini kuanzia  april tatu hadi julai 3 mwaka huu na wangi wameanza kufunguliwa na kuwekwa huru bila kuangalia dini dhehebu kanisa na kabila mbalimbali.
unaweza kuwasiliana na kanisa la EAGT City center na namba  0784367826,0754367826 na 0718267171 pia tembelea  www.pastorkatunzi.blogspot.com au tovuti ya www.eagtcc.org

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

Eagt City Centre Blog 2013. Powered by Blogger.

About Me

My photo
Jicho langu latoka machozi lisokome,wala haliachi;Hata BWANA atakapoangalia. Nakutazama toka mbinguni Maombolezo 3:49-50

Followers

Featured Posts

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget